The Noble Qur'an Encyclopedia
Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languagesThe Women [An-Nisa] - Swahili translation - Rowad Translation Center - Ayah 176
Surah The Women [An-Nisa] Ayah 176 Location Madanah Number 4
يَسۡتَفۡتُونَكَ قُلِ ٱللَّهُ يُفۡتِيكُمۡ فِي ٱلۡكَلَٰلَةِۚ إِنِ ٱمۡرُؤٌاْ هَلَكَ لَيۡسَ لَهُۥ وَلَدٞ وَلَهُۥٓ أُخۡتٞ فَلَهَا نِصۡفُ مَا تَرَكَۚ وَهُوَ يَرِثُهَآ إِن لَّمۡ يَكُن لَّهَا وَلَدٞۚ فَإِن كَانَتَا ٱثۡنَتَيۡنِ فَلَهُمَا ٱلثُّلُثَانِ مِمَّا تَرَكَۚ وَإِن كَانُوٓاْ إِخۡوَةٗ رِّجَالٗا وَنِسَآءٗ فَلِلذَّكَرِ مِثۡلُ حَظِّ ٱلۡأُنثَيَيۡنِۗ يُبَيِّنُ ٱللَّهُ لَكُمۡ أَن تَضِلُّواْۗ وَٱللَّهُ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمُۢ [١٧٦]
Wanakuuliza hukumu ya kisheria, sema: Mwenyezi Mungu anawapa hukumu ya kisheria juu ya kalala (mtu aliyekufa bila ya kuacha mzazi wala mwana). Ikiwa mtu amekufa, naye hana mwana, lakini anaye dada, basi huyo atapata nusu ya alichokiacha. Naye (mwanamume) atamrithi (dada yake) ikiwa hana mwana. Na ikiwa wao ni madada wawili, basi watapata theluthi mbili za alichokiacha. Na wakiwa ndugu wanaume na wanawake, basi wa kiume atapata sehemu iliyo sawa na ya wa kike wawili. Mwenyezi Mungu anawabainishia ili msipotee. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua kila kitu.